Simba yaipania Coastal Union

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th September 2023


Simba yaipania Coastal Union

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally ametamba kuwa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Coastal Union utakuwa maalum kwa klabu hiyo kusahihisha makosa waliyofanya nchini Zambia na kupelekea wakalazimishwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Power Dynamos katika mchezo wa kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika

Alhamisi ya wiki hii Simba itashuka uwanja Uhuru kumenyana na Coastal Union katika mchezo ambao awali ulipaswa kupigwa mwishoni mwa mwezi uliopita

"Mpaka sasa taarifa iliyopo ni kuwa mchezo wetu dhidi ya Coastal Union utapigwa uwanja wa Uhuru, lakini kama kutakuwa na mabadiliko tutatoa taarifa"

"Mchezo huu ni muhimu kwetu kama sehemu ya maandalizi kuelekea mchezo wa marudiano dhidi ya Power Dynamos"

"Kocha wetu (Robertinho) na wachezaji wetu watatumia mchezo huu kujisahihisha kwa kuhakikisha tunaibuka na ushindi mnono kabla ya mchezo wetu dhidi ya Power Dynamos ambao ni lazima tushinde ili tuweze kutinga makundi ya ligi ya mabingwa," alisema Ahmed

Simba inahitaji ushindi dhidi ya Coastal Union ili kurejea katika nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi ambapo Mashujaa Fc inaongoza ikiwa na alama saba baada ya kucheza mechi tatu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.