Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Saidi Yakubu leo amefanya ziara Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam kujionea ukarabati wa uwanja huo ambao utatumika kwenye ufunguzi wa michuano ya African Football League (AFL) Oktoba 20, 2023
Simba itaiwakilisha Tanzania katika michuano hiyo ambayo inafanyika kwa mara ya kwanza barani Afrika ikihusisha timu nane
Simba itacheza mechi ya ufunguzi dhidi ya Al Ahly ya Misri







