Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumanne Septemba 19 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
19 Sep 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumanne Septemba 19 2023

Chelsea na Bayern Munich wanamfuatilia Aaron Ramsdale, 25, baada ya mlinda mlango huyo wa Uingereza na Arsenal kuachwa nje ya mechi ya The Gunners dhidi ya Everton siku ya Jumapili. (Daily Mail)

Manchester United inaandaa ofa ya kumnunua mshambuliaji wa Bayern Munich na Ujerumani Serge Gnabry huku klabu hiyo ikiwa tayari kutoa takriban pauni milioni 52 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28. (Fichajes - kwa Kihispania)

Beki wa Atletico Madrid na Uruguay Jose Maria Gimenez, 28, pia anavutiwa na Manchester United. (FourFourTwo)

Newcastle wanafikiria kutoa ofa ya pauni milioni 52 kumnunua kiungo wa West Ham Lucas Paqueta. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alihusishwa na Manchester City msimu wa joto lakini uhamisho huo ulitibuka kufuatia uchunguzi wa madai ya ukiukaji wa kamari uliofanywa na Mbrazil huyo. (Daily Mail)

Mlinzi wa Uingereza Trent Alexander-Arnold anakaribia kufikia mkataba mpya na Liverpool licha ya Barcelona na Real Madrid kumtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (90min)

Kiungo wa Manchester City na Ureno Bernardo Silva, 29, atagharimu klabu yake inayofuata pauni milioni 50 kutokana na mkataba wake mpya ikiwa ni pamoja na kipengele cha kutolewa. (Fabrizio Romano)

Beki wa Ufaransa Giulian Biancone, 23, amekamilisha uhamisho wa kudumu kutoka Nottingham Forest hadi Olympiacos. (The Athletic -Usajili unahitajika)

Mchezaji wa Liverpool Montevideo Fabricio Diaz, 20, anahamia klabu ya Qatar Al Gharafa huku kiungo huyo wa Uruguay akivutiwa na Brighton na Barcelona. (Fabrizio Romano)

Kiungo wa kati wa Ujerumani Julian Draxler, 29, amejiunga na klabu ya Al Ahli SC ya Qatar kutoka Paris St-Germain kwa mkataba wa kudumu. (Fabrizio Romano)

Beki wa Chelsea mwenye umri wa miaka 19 Muingereza Alfie Gilchrist ameongeza mkataba wake wa mwaka mmoja hadi Juni 2025. (Standard)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
7h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
7h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
8h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
11h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
15h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
15h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
16h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
17h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
18h ago
READ MORE β†’