Wiki mbili zilizopita Klabu ya Singida Fountain Gate ilimtambulisha Ernst Middendorp raia wa Ujerumani kuwa kocha mkuu akichukua nafasi ya Kocha Hans ambaye alikuwa na timu mwanzo wa msimu
Taarifa iliyotoka leo ni kwamba Mwalimu huyo ameomba kuondoka (ameachia ngazi) siku moja baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Future Stars ya Misri mchezo wa CAF CC
Kocha huyo amefanya mazungumzo nakituo cha habari iDiski Times cha Afrika Kusini na kusema ameamua kuachana na Singida FG kufuatia baadhi ya viongozi kuingilia majukumu yake Kwenye mchezo dhidi ya Future Fc
Middendorp alimpanga Gadiel Michael katika eno la kiungo wa ulinzi na kumuweka benchi Morice Chukwu raia wa Nigeria ambaye ndiye anayecheza nafasi hiyo kitendo kilochowakwaza Mabosi wa Singida FG
Mchezo ukiwa unaendelea alipigiwa simu muda wa mapumziko afanye mabadilikona baadae timu ilipata bao moja Baada ya mchezo msimamo wa Viongozi ukawa kama angepanga vizuri kikosi wangeshinda kwa idadai kubwa ya mabao, viongozi walijitetea kwa hoja ya kwamba mwalimu ni mgeni hivyo hawajui vizuri wachezaji wote
Licha ya uongozi wa Singida FG kudai kuwa kocha huyo amepata dharura na atarejea nchini, kulingana na mahojiano aliyofanya huko Afrika Kusini, ni wazi Middendorp huenda hatarejea Singida FG



