Yanga - Local

Gamondi kuwabadilisha Namungo Fc kikosi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
19 Sep 2023
Gamondi kuwabadilisha Namungo Fc kikosi

Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema kikosi chake kimekamilisha maandalizi kuelekea mchezo wa ligi kuu dhidi ya Namungo Fc ambao utapigwa kesho Jumatano katika uwanja wa Azam Complex

Licha ya uchovu na baadhi ya wachezaji kuwa majeruhi, Gamondi amesema anaimani na wachezaji wote, yeyote anaweza kumtumia kwenye mchezo huo na timu ikapata matokeo mazuri

"Jana Tulianza maandalizi kuelekea mchezo wetu na Namungo, tuna baadhi ya wachezaji wana uchovu na wengine wana majeraha lakini nina imani na wachezaji waliopo benchi kwa sababu najua wanaweza kutupa matokeo chanya," alisema Gamondi

Aidha Kocha huyo raia wa Argentina amebainisha kuwa siri ya mwendelezo mzuri wa matokeo ya kikosi chake inatokana na kazi nzuri wanayofanya kwa pamoja kati ya benchi la ufundi na wachezaji

Amesema falsafa yake ni kujenga timu imara ambayo kila mmoja anashiriki na hakuna utegemezi wa mchezaji mmoja mmoja

"Nimeona wengi wakiongelea ubora wa baadhi ya wachezaji lakini kwangu mimi dira yangu sio mchezaji mmoja mmoja bali timu nzima. Ndio maana utagundua timu yetu tunacheza mchezo mzuri, na mchezaji yoyote anaweza kufunga"

"Nimejenga mazingira ya kuwa na timu iliyo na uwiano mzuri kwa kila idara, tazama tumefunga magoli mengi lakini vile vile tumeruhusu goli moja tu katika michezo saba tena bao la penati ambalo ilikuwa kosa letu"

"Sasa ili uwe na uwiano na namna hiyo lazima ujenge timu inayotegemeana na sio timu inayomtegemea mtu fulani kwenye idara fulani"

"Jambo ambalo nimezingatia kwanza ni wachezaji kuheshimiana wenyewe kwa wenyewe, pili wachezaji kuheshimu falsafa zangu, huwezi kuwa kocha mzuri kama wachezaji hawakuheshimu. Kimsingi matokeo chanya ya sasa ni kutokana na jitihada za wachezaji na benchi la ufundi," alisema Gamondi

Kesho Jumatano majira ya saa 1 usiku Yanga itashuka uwanja wa Azam Complex kumenyana na Namnungo Fc katika mchezo ambao matokeo ya ushindi kwa Yanga yatawarudisha kileleni mwa msimamo wa ligi

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
4m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
33m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’