Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Septemba 20 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 20th September 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Septemba 20 2023

Mwenyekiti wa Tottenham Daniel Levy amefichua kuwa klabu hiyo ina kipengele cha kumnunua tena mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane, 30, iwapo ataondoka Bayern Munich. (Fooball.London)

Kane angesubiri hadi msimu ujao wa kiangazi kujiunga na Manchester United kwa uhamisho wa bure kutoka Spurs ikiwa angepewa uhakikisho wa kuhamia Old Trafford. (Mail)

Real Madrid walikuwa wameweka dau la pauni milioni 60 kumnunua Kane kabla ya nahodha huyo wa Uingereza kuhamia Bayern Munich msimu huu huku Paris St-Germain nao wakituma ombi. (The Athletic - Usajili unahitajika)

Kocha wa Brentford Thomas Frank anasema atafikiria kumuuza mshambuliaji wa Uingereza Ivan Toney, 27, mwezi Januari kama bei itakuwa sawa. (Sky Sports)

Klabu za Arsenal, Chelsea na Tottenham zinavutiwa na Toney huku Brentford ikiwa tayari kumruhusu mchezaji huyo kuondoka kwa ada ya £60m. (Mirror)

Arsenal ilituma wasaka vipaji wake kwenye mechi ya Reading ya EFL Trophy dhidi ya Exeter siku ya Jumanne huku The Gunners wakiwa na nia ya kumnunua mshambuliaji Mwingereza Caylan Vickers mwenye umri wa miaka 18 na mlinzi wa New Zealand Tyler Bindon, 18. (Express)

Arsenal pia wanavutiwa na mshambuliaji Mwingereza Jamie Bynoe-Gittens mwenye umri wa miaka 19 katika klabu ya Borussia Dortmund. (Fichajes kupitia Daily Star)

Boca Juniors wana matumaini ya kufikia kandarasi mpya na mlinzi wa Argentina Valentin Barco, 19, licha ya Brighton kumtaka. (90min)

Aston Villa wako kwenye mazungumzo ya kumpa beki wa Uingereza Ezri Konsa, 25, mkataba mpya. (Mail)

Barcelona wameonyesha nia ya kumnunua kiungo wa Royal Antwerp Arthur Vermeeren huku Mbelgiji huyo mwenye umri wa miaka 18 akitajwa kuwa Sergio Busquets ajaye. (90min)

Mmiliki wa AC Milan Gerry Cardinale alikutana na mshambuliaji wa zamani Zlatan Ibrahimovic, 41, kuhusu nafasi ya bodi ya fowadi huyo wa zamani wa Sweden. (Football Italia)

Nahodha wa zamani wa Chelsea John Terry, 42, yuko katika kundi linalotaka kununua asilimia 10 ya hisa katika klabu hiyo huku mmiliki mwenza Todd Boehly akiwa tayari kwa uwekezaji mpya. (Telegraph - usajili unahitajika)

Mshambulizi wa West Ham Michail Antonio, 33, ana nia ya kusalia London Stadium na anataka kusaini mkataba mpya na klabu hiyo. (Football Insider)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.