Mchezo wa ligi kuu ya NBC kati ya Simba dhidi ya Coastal Union ambao utapigwa kesho Alhamisi Septemba 21, utachezwa katika uwanja wa Uhuru kama ratiba ilivyopangwa awali
Kulikuwa na taarifa ya mchezo huo kupelekwa uwanja wa Azam Complex, lakini kulingana na ratiba iliyotolewa na Bodi ya Ligi, mchezo huo umebaki dimba la Uhuru ambalo Simba walichagua kulitumia wakati uwanja wa Benjamin Mkapa ukiendelea na ukarabati

Kikosi cha Simba kilirejea juzi kutoka Zambia baada ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Power Dynamos uliomalizika kwa matokeo ya sare ya mabao 2-2
Wekundu hao wa Msimbazi waliingia moja kwa moja kambini na leo watakamilisha maandalizi yao tayari kuwakabili Coastal Union ambao tayari wako jijini Dar es salaam



