Simba - Coastal - Azam - Singida - Local

Simba, Azam Fc viwanjani Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Sep 2023
Simba, Azam Fc viwanjani Ligi Kuu

Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo michezo miwili inatarajiwa kupigwa jijini Dar es salaam

Wekundu wa Msimbazi Simba wanarejea katika mbio za ubingwa msimu huu wakiikaribisha Coastal Union katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Uhuru saa 10 jioni

Wakati Simba ikiwa inasaka ushindi wake wa tatu msimu huu, hali ni tofauti kwa wapinzani wao Coastal Union ambao wanasaka ushindi wa kwanza

Mara ya mwisho timu hizo zilipokutana kwenye uwanja wa Uhuru msimu uliopita, Simba iliibuka na ushindi wa mabao 3-1

Matarajio ya mashabiki wa Simba ni kuona timu yao inaendeleza wimbi la ushindi katika msimu ambao wanautaka ubingwa wa Ligi Kuu

Mchezo mwingine kati ya Azam Fc dhidi ya Singida FG utapigwa saa 1 usiku katika uwanja wa Azam Complex

Azam Fc ilioanza vyema msimu huu kwa ushindi katika mechi mbili zilizopita, inasaka ushindi wa tatu wakati Singida FG wameambulia alama mbili tu katika mechi zao mbili zilizopita hivyo ni mchezo ambao watahitaji ushindi

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
38m ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
50m ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
1h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
4h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
8h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
9h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
10h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
11h ago
READ MORE β†’