Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo michezo miwili inatarajiwa kupigwa jijini Dar es salaam
Wekundu wa Msimbazi Simba wanarejea katika mbio za ubingwa msimu huu wakiikaribisha Coastal Union katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Uhuru saa 10 jioni
Wakati Simba ikiwa inasaka ushindi wake wa tatu msimu huu, hali ni tofauti kwa wapinzani wao Coastal Union ambao wanasaka ushindi wa kwanza
Mara ya mwisho timu hizo zilipokutana kwenye uwanja wa Uhuru msimu uliopita, Simba iliibuka na ushindi wa mabao 3-1
Matarajio ya mashabiki wa Simba ni kuona timu yao inaendeleza wimbi la ushindi katika msimu ambao wanautaka ubingwa wa Ligi Kuu
Mchezo mwingine kati ya Azam Fc dhidi ya Singida FG utapigwa saa 1 usiku katika uwanja wa Azam Complex
Azam Fc ilioanza vyema msimu huu kwa ushindi katika mechi mbili zilizopita, inasaka ushindi wa tatu wakati Singida FG wameambulia alama mbili tu katika mechi zao mbili zilizopita hivyo ni mchezo ambao watahitaji ushindi



