Refa kutoka Gabon kuchezesha Yanga vs Al Merrikh

Joel JJ By Joel JJ β€’ 22nd September 2023


Refa kutoka Gabon kuchezesha Yanga vs Al Merrikh

Wiki ijayo Septemba 30 2023 Yanga itakuwa ikipigania nafasi adimu ya kutinga hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika katika mchezo wa marudiano dhidi ya Al Merrikh ya Sudan

Huu ni mchezo muhimu sana kwa Yanga kushinda au hata kupata matokeo ya sare ili kumaliza ukame wa kutocheza hatua ya makundi ya michuano hiyo kwa zaidi ya miaka 24

Mwamuzi aliyepewa jukumu la kusimamia mchezo huo ni Tanguy Mebiani kutoka nchini Gabon

Yanga ikiwa mbele kwa ushindi wa mabao 2-0 waliopata nchini Rwanda wako katika nafasi nzuri ya kutinga hatua ya makundi

Licha ya nafasi yao, kocha mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema wanajiandaa kikamilifu na hawafikirii matokeo ya mchezo wa kwanza

Gamondi amesema bado kikosi chake hakijafuzu na amewataka wachezaji wake wasibweteke kwani kama wao waliweza kufunga mabao mawili ugenini hata wapinzani wao wanaweza kufanya hivyo jijini Dar es salaam

Al Merrikh wameanza 'mind games' mapema ambapo juzi zilisambaa taarifa kutoka Rwanda kuwa timu hiyo imewaondoa wachezaji 11 kikosini wakidaiwa kutokuwa sawa kisaikolojia wakiathiriwa na vita inayoendelea nchini kwao Sudan

Hata hivyo hizi zinaweza kuwa mbinu tu ili kuwafanya Yanga waamini mchezo wa pili utakuwa rahisi kwao


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.