Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema jambo muhimu kwa Simba msimu huu ni kutimiza malengo yake
Ahmed ametoa kauli hiyo baada ya kuibuka kundi la wachambuzi na baadhi ya mashabiki huko mitandano wakidai hawavutiwi vile Simba inacheza licha ya kupata ushindi katika mechi zake
Ahmed amesema msimu uliopita Simba iliongoza katika takwimu za kucheza vizuri pamoja na kufunga mabao mengi lakini mwisho wa siku hawakushinda kombe lolote
"Mpira wa miguu kilele chake huwa ni ushindi, kwenye Ligi tumechukua alama tatu dhidi ya Mtibwa Sugar, Dodoma Jiji na Coastal Union. Kwa hiyo ukija kwenye malengo, bado tupo kwenye malengo ambayo ni kushinda mechi kadiri tuwezavyo"
"Watu wanataka timu ifunge magoli mengi, msimu uliopita tulifunga magoli mengi na hatukuwa mabingwa. Huyu ambaye anasema tunashinda lakini hatuna furaha, itakuaje kama tutaendelea kushinda na kuwa mabingwa, atakuja kusema hana furaha ya ubingwa?"
"Nadhani kama Simba msimu huu tunapaswa kuishi kwenye malengo makuu ambayo ni kushinda kila mechi," alisema Ahmed



