Jana Kiungo Mtanzania anayecheza Chippa United inayoshiriki ligi kuu ya Afrika kusini 'PSL' Baraka Gamba Majogoro alitwaa tuzo ya Mchezaji bora wa mechi dhidi ya Super Sport United
Baraka ambaye anatumika katika eneo la kiungo cha ukabaji aliisaidia Chippa United kupata ushindi wa 1-0 katika muendelezo wa michezo ya ligi kuu ya Afrika kusini
Majogoro amekuwa chaguo la kwanza katika kikosi cha Chippa akipewa nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza
Chippa United inashika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi kuu ya Afrika Kusini



