Majogoro anaendelea kutamba Afrika Kusini

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th September 2023


Majogoro anaendelea kutamba Afrika Kusini

Jana Kiungo Mtanzania anayecheza Chippa United inayoshiriki ligi kuu ya Afrika kusini 'PSL' Baraka Gamba Majogoro alitwaa tuzo ya Mchezaji bora wa mechi dhidi ya Super Sport United

Baraka ambaye anatumika katika eneo la kiungo cha ukabaji aliisaidia Chippa United kupata ushindi wa 1-0 katika muendelezo wa michezo ya ligi kuu ya Afrika kusini

Majogoro amekuwa chaguo la kwanza katika kikosi cha Chippa akipewa nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza

Chippa United inashika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi kuu ya Afrika Kusini


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.