Yanga - Local

Al Merrikh kutua leo, kuikabili Yanga Jumamosi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Sep 2023
Al Merrikh kutua leo, kuikabili Yanga Jumamosi

Klabu ya Al Merrikh kutoka Sudan inatarajiwa kuwasili nchini leo kuelekea mchezo wa mkondo wa pili wa kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Siku ya Jumamosi Septemba 30, Yanga itachuana na Al Merrikh katika mchezo utakaofanyika uwanja wa Azam Complex, saa 1 usiku

Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari jana, Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe alisema Merrikh watawasili nchini leo Alasiri na Rwandan Air

Al Merrikh wamekuwa mapema kuonyesha 'wanautaka' mchezo huo licha ya kuwa wako nyuma kwa mabao 2-0 ushindi ambao Yanga waliupata kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa Rwanda

Jumamosi Yanga itahitaji kushinda au matokeo yoyote ya sare kuweza kutinga hatua ya makundi

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema kikosi chao kinaendelea vyema na maandalizi kuelekea mchezo huo ambao wamepania kuibuka na ushindiΒ 

"Maandalizi kuelekea mchezo dhidi ya AL Merrikh yanaendelea vizuri, jana tulikuwa na session moja na leo tuna session mbili, asubuhi wachezaji wamefanya mazoezi na pia watafanya jioni"

"Tumezisikia kauli za kocha Al Merrikh anasema Yanga inaogopwa barani Afrika lakini sisi tunamwambia asitutoe kwenye reli, tunamsubiri aje uwanja wa Azam Complex tupambane nae katika mchezo ambao tunajua utakuwa sio rahisi," alisema Kamwe

Kamwe alitangaza viingilio vya mchezo huo VIP A ni Tsh 50,000/-, VIP B ni Tsh 20,000/- na Mzunguuko ni Tsh 10,000/-

Pia kutakuwa na tiketi za Royal zinazopatikana kwa Tsh 100,000/-

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
2h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
6h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
6h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
7h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
8h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
8h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
9h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
9h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
22h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’