Mshambuliaji raia wa Nigeria Victor Osimhen amefuta picha na video zote za Napoli kwenye page yake ya Instagram hii ni kutokana na video ya TikTok iliyopostiwa na Napoli ikionesha kumdhihaki baada ya kukosa penati kwenye mchezo wa Serie A dhidi ya Bologna uliopigwa juzi na kumalizika kwa matokeo ya suluhu
Aidha Mwanasheria wa mchezaji huo ametangaza adhma ya kuwachukulia hatua Napoli Fc akieleza kitendo hicho kimevuruga saikolojia ya mteja wake
Napoli waliweka video hiyo ya dhihaka katika ukurasa rasmi wa klabu hiyo na kuondoa baada ya muda mfupi
Ni kawaida kwa wachezaji kutoka Afrika kukumbana na kadhia za ubaguzi wa rangi Italia, tukio alilofanyiwa Osimhen lina vinasaba vya ubaguzi
Huenda mshambuliaji huyo akaondoka katika dirisha la usajili wa majira ya baridi. Chelsea inapewa nafasi kubwa ya kuinasa saini yake endapo ataachana na Napoli.



