Tanzania, Kenya, Uganda kuandaa Afcon 2027

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th September 2023


Tanzania, Kenya, Uganda kuandaa Afcon 2027

Rasmi Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limepitisha mataifa ya Tanzania, Kenya na Uganda kuandaa michuano ya Afcon 2027

Nchi hizo ziliwasilisha ombi walilobatiza jina la Pamoja Bid na itakuwa mara ya kwanza ukanda wa Afrika Mashariki kuandaa michuano hiyo mikubwa ya soka Afrika

Kamati ya Utendaji CAF imetangaza uamuzi huo nchini Misri leo, pia Morocco imechanguliwa kuandaa Afcon 2025

Kwa kuandaa michuano hiyo maana yake ni kuwa Tanzania, Kenya na Uganda zimejihakikishia tiketi ya kushiriki michuano hiyo na jukumu la Mataifa hayo ni kuhakikisha wanaandaa vyema timu zao ili kuhakikisha kombe la Afcon 2027 linabaki Afrika Mashariki


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.