Meneja wa Brighton Roberto de Zerbi na Xabi Alonso wa Bayer Leverkusen wanawania kuchukua nafasi ya Carlo Ancelotti iwapo ataondoka Real Madrid mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu huu. (Cadena Ser – In Spanish)
Kuna hisia ndani ya Manchester United kwamba uhusiano kati ya meneja Erik ten Hag na winga wa Uingereza Jadon Sancho, 23, hauwezi kurekebishwa. (I) Vilabu vya Saudi Arabia vitaongoza mbio za kumsaka Victor Osimhen mbele ya Real Madrid na Chelsea iwapo mshambuliaji huyo wa Nigeria mwenye umri wa miaka 24 atashinikiza kuondoka Napoli mwezi Januari. (Mail)
Sevilla wamekuwa wakimfuatilia kiungo Hannibal Mejbri, 20, lakini Manchester United wanapanga kufanya mazungumzo ya kandarasi na mchezaji huyo wa kimataifa wa Tunisia hivi karibuni ili kumbakisha Old Trafford. (Fabrizio Romano)
Manchester United pia wanapanga mazungumzo na meneja Erik ten Hag kuhusu mkataba mpya (90Min)
Chelsea wako sokoni kutafuta beki mpya wa kushoto, huku mchezaji wa kimataifa wa Italia wa Inter Milan mwenye umri wa miaka 25 Federico Dimarco na beki wa AC Milan wa Ufaransa Theo Hernandez, 25, wakiwa kwenye orodha yao fupi. (Calciomercato – In Itali)
Sheffield United wamezungumza na kocha wa zamani Chris Wilder kuhusu uwezekano wa kuchukua nafasi ya Paul Heckingbottom kwa kipindi cha pili cha kuinoa klabu hiyo. (Football Insider) Roma wanafikiria kumnunua mlinzi wa Tottenham, 29, Eric Dier, Januari. (Calciomercato – In Italy)
Hatima ya kifedha ya Everton inaweza kuwa shakani ikiwa uchukuaji wa kampuni ya uwekezaji yenye makao yake makuu nchini Marekani ya 777 Partners hautapitishwa. (Guardian)
777 Partners ina uhakika wa kufaulu mtihani wa wamiliki na wakurugenzi wa Ligi ya Premia, na imeanza mazungumzo na makundi ya mashabiki wa Everton ili kujaribu kupunguza wasiwasi wa wafuasi wake kuhusu pendekezo la kuinunua (I) Newcastle walimaliza mkataba wao wa jezi na mtengenezaji wa jezi Caste mapema kutokana na wasiwasi kuhusu ubora wa bidhaa zao. (Subscription Required)
BBC



