Baada ya TFF kutoa taarifa ya kufungiwa kusajili kwa klabu ya Tabora United kutokana kudaiwa na aliyekuwa mchezaji wao Asante Kwasi, Mtendaji Mkuu wa Tabora United Thabit Kandoro amesema mchezaji huyo atalipwa
Kandoro amesema madai ya Kwasi wanatarajia kuyalipia mara baada ya kumaliza mchezo wao dhidi ya Coastal Union
"Hamna Shida yoyote tutamlipa, awali tulikuwa na makubaliano ya malipo yake Asante Kwasi na tulikuwa tunamlipa kidogo kidogo"
"Lakini mchezaji ameona tumefikisha mwisho kumalizia deni lake, naona kaenda kulalamika kuwa hela iliyobaki ni ndogo bora tuilipe yote," alisema Kandoro
Tabora United imekumbana na rungu la kufungiwa na FIFA mara tatu katika kipindi cha miezi miwili iliyopita kutokana na malimbikizo ya madeni kutoka kwa wachezaji na makocha wake wa zamani



