Tabora United kumlipa Kwasi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 29th September 2023


Tabora United kumlipa Kwasi

Baada ya TFF kutoa taarifa ya kufungiwa kusajili kwa klabu ya Tabora United kutokana kudaiwa na aliyekuwa mchezaji wao Asante Kwasi, Mtendaji Mkuu wa Tabora United Thabit Kandoro amesema mchezaji huyo atalipwa

Kandoro amesema madai ya Kwasi wanatarajia kuyalipia mara baada ya kumaliza mchezo wao dhidi ya Coastal Union

"Hamna Shida yoyote tutamlipa, awali tulikuwa na makubaliano ya malipo yake Asante Kwasi na tulikuwa tunamlipa kidogo kidogo"

"Lakini mchezaji ameona tumefikisha mwisho kumalizia deni lake, naona kaenda kulalamika kuwa hela iliyobaki ni ndogo bora tuilipe yote," alisema Kandoro

Tabora United imekumbana na rungu la kufungiwa na FIFA mara tatu katika kipindi cha miezi miwili iliyopita kutokana na malimbikizo ya madeni kutoka kwa wachezaji na makocha wake wa zamani


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.