Wapinzani wa Simba katika mchezo wa ligi ya Mabingwa Power Dynamos wamewasili nchini usiku wa kuamkia leo tayari kwa mchezo utakaopigwa Jumapili katika uwanja wa Azam Complex
Akizungumza baada ya kutua JNIA, Meneja wa timu hiyo amesema wamekuja Tanzania kusaka ushindi
"Tumejipanga vyema na tuna uhakika wa ushindi kwenye mchezo wetu wa marejeano Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Simba utakaochezwa Oktoba 01, 2023 katika uwanja wa Azam Complex," alisema
Mchezo wa kwanza uliochezwa katika Uwanja wa Levy Mwanawasa Zambia uliisha kwa sare ya mabao 2-2 mabao ya Simba yakifungwa na Clatous Chama. Katika mchezo huo ili kufuzu hatua ya Makundi Simba atatakiwa kupata ushindi wowote au sare ya 0-0 na 1-1 huku Power dynamos nao wakihitaji Ushindi au sare ya kuanzia mabao 3-3 ili wasonge mbele



