Yanga - Local

Gamondi awapania Al Merrikh

Joel JJ By Joel JJ
29 Sep 2023
Gamondi awapania Al Merrikh

Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema wamekuwa na muda wa kutosha kujiandaa na mchezo wa mkondo wa pili kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Al Merrikh

Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo kuelekea mchezo huo utakaopigwa Jumamosi, Septemba 30 saa 1 usiku, Gamondi amesema wachezaji wote wako tayari kupambana katika mchezo huo muhimu katika historia ya Yanga

"Tumekuwa na muda wa kutosha kujiandaa na mchezo huu. Maandalizi ni mazuri, tuko tayari kucheza kandanda safi na kuwapa furaha Wananchi kwenye mchezo huu"

"Moja ya mambo yaliyonileta Yanga ni pamoja na michuano ya ligi ya mabingwa. Hii ndio michuano mikubwa zaidi barani Afrika kwa ngazi ya klabu. Nafahamu tuna zaidi ya miaka 25 hatujacheza hatua hii"

"Malengo na mipango yetu ni kuona tunapata matokeo mazuri na kufuzu hatua ya makundi. Pamoja na ushindi tuliopata mchezo wa kwanza, tutacheza mchezo huu kama matokeo ni 0-0 tutakuja uwanjani kupambana kama ni fainali na nitatumia tiimu yangu bora zaidi ili kuhakikisha tunapata matokeo tunayohitaji," alisema Gamondi

Gamondi amesema wachezaji wake wote wako tayari kwa mchezo huo wakiwa na ari, morali kubwa jukumu lake ni kuchagua wachezaji 11 ambao watakuwa na jukumu la kuhakikisha Yanga inaibuka na ushindi ili kutinga hatua ya makundi

More Stories

BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
13m ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
27m ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
1h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
1h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
1h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
1h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
2h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
4h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
14h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
14h ago
READ MORE →