Yanga imetinga hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Al Merrikh katika mchezo wa mkondo wa pili uliopigwa uwanja wa Azam Complex
Bao lililofungwa na Clement Mzize kwenye kipindi cha pili liliihakikishia Yanga ushindi wa jumla wa mabao 3-0
Mzize aliweka kambani bao hilo kwa kichwa akiunganisha krosi ya Joyce Lomaliza Mutambala
Ilikuwa ni Aziz Ki Day iliyofana mashabiki wa Yanga wakifurika dimba la Azam Complex kuhanikiza ushindi huo
Ni takribani miaka 25 imepita tangu Yanga icheze hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa, Wananchi wamerejea katika hatua hiyo



