Simba yatinga makundi Ligi ya Mabingwa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st October 2023


Simba yatinga makundi Ligi ya Mabingwa

Simba imekata tiketi hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika licha ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Power Dynamos katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex

Power Dynamos walitangulia kwa bao la mapema kwenye kipindi cha kwanza kabla ya Simba kusawazisha kwenye dakika ya 69 kwa bao la kujifunga mlinzi wa Power Dynamos

Ulikuwa mchezo wa vipindi viwili kipindi cha kwanza Simba ilicheza taratibu lakini kasi iliongezeka kwenye kipindi cha pili hasa baada ya kuingia nahodha John Bocco na Willy Onana

Simba imetinga makundi kwa faida ya bao la ugenini licha ya matokeo ya sare ya mabao 3-3

Simba sasa inaungana na Yanga kuwa timu mbili zilizotinga hatua ya makundi ligi ya mabingwa kutoka Tanzania kwa mara ya kwanza


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.