Simba imekata tiketi hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika licha ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Power Dynamos katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex
Power Dynamos walitangulia kwa bao la mapema kwenye kipindi cha kwanza kabla ya Simba kusawazisha kwenye dakika ya 69 kwa bao la kujifunga mlinzi wa Power Dynamos
Ulikuwa mchezo wa vipindi viwili kipindi cha kwanza Simba ilicheza taratibu lakini kasi iliongezeka kwenye kipindi cha pili hasa baada ya kuingia nahodha John Bocco na Willy Onana
Simba imetinga makundi kwa faida ya bao la ugenini licha ya matokeo ya sare ya mabao 3-3
Simba sasa inaungana na Yanga kuwa timu mbili zilizotinga hatua ya makundi ligi ya mabingwa kutoka Tanzania kwa mara ya kwanza



