Madeni yaiponza Tabora United, yafungiwa tena na FIFA

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd October 2023


Madeni yaiponza Tabora United, yafungiwa tena na FIFA

Klabu ya Tabora United inayoshiriki Ligi Kuu Bara imefungiwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) baada ya wachezaji wa wawili Emmanuel Lamptey na Collins Gymfi kushinda kesi za madai dhidi ya klabu hiyo

Wachezaji hao raia wa Ghana walifungua kesi FIFA wakidai malipo ya ada ya usajili (sign on fee) na malimbikizo ya mishahara

Tabora United iltakiwa iwe imewalipa ndani ya siku 45 tangu uamuzi huo ulipoletwa, lakini haikutekeleza hukumu hiyo

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) pia limetangaza kuifungia Tabora United kufanya usajili wa ndani mpaka pale itakapomalizana na wachezaji hao


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.