Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Oktoba 04 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th October 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Oktoba 04 2023

Kuna uwezekano mkubwa wa winga wa England Jadon Sancho kuondoka Manchester United wakati wa uhamisho wa Januari, huku Borussia Dortmund wakipania kumrejesha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 kwenye ligi kuu ya Ujerumani maarufu Bundesliga. (Sky Germany)

Beki wa Everton na England wa chini ya miaka 21 Jarrad Branthwaite, 21, yuko kwenye orodha ya wachezaji wanaonyatiwa na United katika dirisha lijalo la uhamisho. (Mail)

Frank Lampard yuko tayari kuzungumza na Rangers kuhusu nafasi iliyo wazi ya meneja huku klabu hiyo ikianza mchakato wa kutafuta mbadala wa kudumu wa Michael Beale. (Telegraph)

Gwiji wa Argentina Lionel Messi, 36, ameripotiwa kutaka kurejea katika klabu yake ya kwanza, Newell's Old Boys, mkataba wake na Inter Miami utakapokamilika 2025. (Mirror)

Leeds, Leicester na Burnley wameandika barua ya pamoja kwa wanaotarajiwa kuwa wamiliki wapya wa Everton, 777 Partneres, kwamba wanakusudia kuishtaki klabu hiyo kwa £300m iwapo watapatikana na hatia ya kukiuka sheria za matumizi ya Ligi Kuu ya Uingereza. (Mail)

Chelsea wanapewa nafasi kubwa ya kumsajili mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen, 24, kutoka Napoli msimu ujao, huku Evan Ferguson wa Brighton, 18, na Ivan Toney wa Brentford, 27, pia akiwa miongoni mwa washambuliaji wanaolengwa. (Caught Offside)

Barcelona inatarajiwa kupokea ofa ya wachezaji wote wa kikosi cha kwanza kwani klabu hiyo bado inazidisha kikomo cha matumizi ya kila mwaka ya euro 270m (£234m) iliyowekwa na La Liga. (Sport - kwa Kihispania)

Kiungo wa kati wa Croatia Luka Modric, ambaye amekuwa akihusishwa na kuhamia Inter Miami, anaweza kuondoka Real Madrid huku klabu hiyo ya Uhispania ikihisi kwamba utenda kazi wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 38 umeshuka. (Football Espana)

Beki wa Bayer Leverkusen Mholanzi Jeremie Frimpong, 22, anatazamiwa kusaini mkataba mpya na klabu hiyo ya Ujerumani, na hivyo kuongeza thamani ya uhamisho wa mchezaji anayevutia Manchester United na Real Madrid. Hilo linaweza pia kufaidisha klabu yake ya zamani ya Celtic, ambayo ina kipengele cha kuuza cha 30%. (Daily Record)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.