Yanga - Ihefu - Local

Ihefu Fc yaendeleza ubabe dhidi ya Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Oct 2023
Ihefu Fc yaendeleza ubabe dhidi ya Yanga

Tunaweza kusema uwanja wa Highland Estates sio eneo salama kwa Yanga baada ya leo tena kupoteza mchezo dhidi ya Ihefu Fc kwa kufungwa mabao 2-1

Ni vilevile kama ilivyokuwa msimu uliopita, Pacome Zouzoua aliitanguliza Yanga mapema kwenye dakika ya sita lakini Ihefu Fc wakarejea mchezoni baada ya makosa ya kufanyika kwenye eneo la Yanga

Nahodha wa Yanga Bakari Mwamnyeto alifanya madhambi karibu na eneo la hatari baada ya kuchelewa kuondoa mpira kwenye eneo la hatari

Mpira wa adhabu kutoka Never Tigere ulimshinda mlinda lango wa Yanga Djigui Diarra akishindwa kuondosha eneo la hatari na Lenny Kissu kuweka bao kimiani

Bao la pili la Ihefu Fc lilifungwa na Charles Ilanfya baada ya shambulizi la kushitukiza

Huu ni ushindi wa pili kwa Ihefu Fc msimu huu katika mechi nne walizocheza, ukiwa pia ni ushindi wa pili katika uwanja wao wa nyumbani

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
7h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
7h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
8h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
11h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
15h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
15h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
16h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
17h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
18h ago
READ MORE β†’