Yanga, Simba zakwepana makundi CAF CL

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th October 2023


Yanga, Simba zakwepana makundi CAF CL

Droo ya hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika imefanyika leo huko Afrika  Kusini ambapo Yanga imepangwa kundi D na watani zao Simba wakipangwa kundi B

Katika kundi D Yanga itachuana na Al Ahly (Misri), Medeama (Ghana) na CR Belouizdad (Algeria)

Kundi B ambalo wamo Simba lina Jwaneng Galaxy, Asec Mimosas na Wydad Athletic

Kundi A lina Nouadhibou, TP Mazembe, Mamelodi Sundowns na Pyramids

Kundi C lina Etoile Du Sahel,  Al Hilal, Petro Atletico na Esperance

Mechi za hatua ya makundi zitaanza kupigwa Novemba 24/25 mwaka huu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.