Droo ya hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika imefanyika leo huko Afrika Kusini ambapo Yanga imepangwa kundi D na watani zao Simba wakipangwa kundi B
Katika kundi D Yanga itachuana na Al Ahly (Misri), Medeama (Ghana) na CR Belouizdad (Algeria)
Kundi B ambalo wamo Simba lina Jwaneng Galaxy, Asec Mimosas na Wydad Athletic
Kundi A lina Nouadhibou, TP Mazembe, Mamelodi Sundowns na Pyramids
Kundi C lina Etoile Du Sahel, Al Hilal, Petro Atletico na Esperance
Mechi za hatua ya makundi zitaanza kupigwa Novemba 24/25 mwaka huu



