Ligi Kuu ya NBC imeendelea leo kwa mechi mbili kupigwa ambapo mabingwa watetezi Yanga walikuwa mkoani Mwanza kuikabili Geita Gold katika uwanja wa CCM Kirumba
Yanga imerejesha furaha ya mashabiki wake baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Geita Gold
Mabao ya Yanga yalifungwa na Pacome Zouzoua, Stephane Aziz Ki na Maxi Nzengeli
Ulikuwa mchezo ambao Geita Gold walijihami zaidi kwenye kipindi cha kwanza lakini haikuwasaidia kwani mpaka mapumziko walikuwa nyuma kwa mabao 2-0
Ushindi huo umeirejesha Yanga kwenye nafasi ya pili baada ya kufikisha alama 12, sawa na Simba lakini Yanga ina uwiano mzuri wa mabao
Simba ina mchezo mmoja wa kiporo dhidi ya Singida FG utakaopigwa uwanja wa LITI kesho Jumapili
Katika mchezo mwingine, KMC imeichapa Ihefu Fc bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru
KMC imefikisha alama 10 na kusogea mpaka nafasi ya pili



