Yanga yatakata Mwanza, Ihefu chali mbele ya KMC

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th October 2023


Yanga yatakata Mwanza, Ihefu chali mbele ya KMC

Ligi Kuu ya NBC imeendelea leo kwa mechi mbili kupigwa ambapo mabingwa watetezi Yanga walikuwa mkoani Mwanza kuikabili Geita Gold katika uwanja wa CCM Kirumba

Yanga imerejesha furaha ya mashabiki wake baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Geita Gold

Mabao ya Yanga yalifungwa na Pacome Zouzoua, Stephane Aziz Ki na Maxi Nzengeli

Ulikuwa mchezo ambao Geita Gold walijihami zaidi kwenye kipindi cha kwanza lakini haikuwasaidia kwani mpaka mapumziko walikuwa nyuma kwa mabao 2-0

Ushindi huo umeirejesha Yanga kwenye nafasi ya pili baada ya kufikisha alama 12, sawa na Simba lakini Yanga ina uwiano mzuri wa mabao

Simba ina mchezo mmoja wa kiporo dhidi ya Singida FG utakaopigwa uwanja wa LITI kesho Jumapili

Katika mchezo mwingine, KMC imeichapa Ihefu Fc bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru

KMC imefikisha alama 10 na kusogea mpaka nafasi ya pili


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.