Leo Jumamosi asubuhi Simba imecheza mechi ya kirafiki dhidi ya Dar City kwenye uwanja wake wa Mo Simba Arena, Bunju - Dar es Salaam na kuibuka na ushindi wa mabao 5-1, huku kipa wake Aishi Manula akirejea langoni.
Mchezo huo ni wa kwanza kwa Manula msimu huu kwani kabla ya hapo alikuwa nje ya uwanja akiuguza majeraha ya nyonga aliyoyapata Aprili 7, mwaka huu kwenye mechi ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (ASFC), dhidi ya Ihefu katika Uwanja wa Azam Complex.
Katika mchezo wa leo, Manula alianza langoni Simba akicheza kwa dakika 40, kabla ya kufanyiwa mabadiliko na nafasi yake kuchukuliwa na Hussein Abel ambaye naye bado hajapata muda wa kutosha kucheza ndani ya kikosi hicho tangu asajiliwe mwanzoni mwa msimu akitokea KMC.
Kurejea kwa Manula ni taarifa njema kwa Simba kuelekea mchezo wa AFL dhidi ya Al Ahly ambao utapigwa Ijumaa, Otoba 20 katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Manula huenda akawa tayari kuwakabili Al Ahly katika mchezo huo



