Katwila kuibukia Singida BS

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th October 2023


Katwila kuibukia Singida BS

Wakati klabu ya Ihefu na Kocha Zuberi Katwila wakithibitisha kufikia tamati kwa mkataba baina yao kwa makubaliano binafsi, imeelezwa kuwa kocha huyo anaenda kujiunga na Singida Big Stars kama kocha msaidizi

Katwila ni miongoni mwa makocha wanaotua Singida BS kusuka benchi jipya la ufundi litakaloongozwa na kocha wa kigeni ambaye atatangazwa hivi karibuni, huku timu hiyo ikiwa katika mpango wa kuachana na Mathias Lule na Thabo Senong waliokuwa wanaiongoza baada ya kuondoka kwa kocha mkuu Ernst Middendorp

"Kuna kocha kutoka Brazil anakuja kuchukua nafasi ya kocha mkuu na msaidizi wake atakuwa ni Zuberi Katwila. Mpango wa kumchukua Katwila ulianza muda mrefu, ndio maana tulianza kumchukua kocha wa makipa, Peter Manyika," kimefichua chanzo ndani ya Singida

Leo Jumamosi asubuhi Ihefu ilitangaza kuachana na Katwila aliyekuwa akiinoa kwa miaka mitatu tangu Oktoba 2020 alipojiunga akitokea Mtibwa Sugar, klabu aliyowahi kuichezea


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.