Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' iko Saudi Arabia ambapo leo Jumapili, itachuana na Sudan katika mchezo wa Kimataifa wa kirafiki
Mchezo huo ambao uko kwenye kalenda ya FIFA, matokeo yake yana umuhimu mkubwa kwenye kuboresha viwango 'ranking' za FIFA
Stars ilitua Saudi Arabia jana tayari kwa mchezo huo ambao utapigwa saa 1 usiku
Kocha Mkuu wa Stars Adel Amrouche alisafiri na kikosi cha wachezaji 28




