Yanga - Local

Gamondi anazihitaji alama tatu za Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ
16 Oct 2023
Gamondi anazihitaji alama tatu za Azam Fc

Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema kikosi chake kitakuwa tayari kuikabili Azam Fc kwenye mchezo wa ligi kuu utakaopigwa Jumapili, Oktoba 22 katika uwanja wa Azam Complex

Mchezo huo umerudishwa nyuma baada ya mabadiliko ya ratiba yaliyofanywa na Bodi ya Ligi, awali ulipangwa kupigwa Oktoba 25

Gamondi amesema wamekaa muda mrefu pasipo kucheza mechi hivyo mchezo huo kurudishwa nyuma ni jambo jema

"Nimefurahishwa na mabadiliko ya ratiba, kwani awali nilikuwa naumiza kichwa namna ya kupata mechi ya kirafiki ili kuwajenga kimwili na kiushindani wachezaji ambao wamekaa nje ya uwanja kwa muda bila kucheza," alisema kocha huyo raia wa Argentina

Aidha Gamondi amesema anaamini wachezaji walio kwenye majukumu ya timu za Taifa watarejea kwa wakati tayari kwa mchezo huo

"Djigui Diarra, Stephane Aziz Ki na Khalid Aucho wanacheza mechi za mwisho za kirafiki wakitumikia timu za taifa, Oktoba 18 nimewaambia warudi siku inayofuata ili kujiandaa na mchezo huo kwani ni mchezo mgumu na wenye ushindani mkubwa"

Nyota wa Yanga waliokuwa timu ya Taifa ya Tanzania wanatarajia kurejea nchini leo baada ya kukamilisha ratiba ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Sudan uliopigwa Saudi Arabia jana na kumalizika kwa sare ya bao 1-1

More Stories

BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
15m ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
29m ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
1h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
1h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
1h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
1h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
2h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
4h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
14h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
14h ago
READ MORE →