Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Oktoba 18 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 Oct 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Oktoba 18 2023

Newcastle United wanatayarisha ofa ya kumnunua kiungo wa kati wa Manchester City na Uingereza Kalvin Phillips, 27. (Mail)

Bayern Munich pia wamezungumza na City kuhusu hali ya Phillips, lakini kiungo wa Fulham na Ureno Joao Palhinha, 28, anasalia kuwa mlengwa mkuu wa klabu hiyo ya Ujerumani. (90 min)

Mkurugenzi wa michezo wa Barcelona Deco amewasiliana na mawakala wa Frenkie de Jong kujadili mpango wa kurefusha kandarasi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, lakini kiungo huyo kimataifa wa Uholanzi hana haraka ya kuanza mazungumzo. (Sport - kwa Kihispania)

Deco anasema itakuwa vigumu kwa Barcelona kuongeza wachezajiwapya kwenye kikosi chao wakati wa usajili wa Januari kwa sababu ya hali ya kifedha ya klabu hiyo. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania)

Liverpool ni miongoni mwa klabu kadhaa za Ligi ya Premia zinazomsaka mshambuliaji wa Ujerumani Jamal Musiala, 20, ambaye mkataba wake na Bayern Munich utaendelea hadi 2026. (Sport Bild - kwa Kijerumani)

Liverpool ilituma maskauti kumtazama mlinzi wa Ureno na Sporting Goncalo Inacio, 22, wakati wa mechi ya nchi yake dhidi ya Bosnia-Herzegovina. (90 min)

Kikosi cha Jurgen Klopp pia ni miongoni mwa klabu kadhaa za Ligi Kuu ya Uingereza zinazomfuatilia kwa karibu kiungo wa Schalke Assan Ouedraogo, 17. (Sky Sports Germany).

Mwekezaji mpya mtarajiwa wa Manchester United Sir Jim Ratcliffe alitilia shaka kuajiriwa kwa klabu hiyo ilipotembelea Old Trafford mwezi Machi, akitumia ununuzi wa kiungo wa Brazil Casemiro, 31, kutoka Real Madrid mnamo Agosti 2022 kama mfano. (Guardian)

Ununuzi wa Ratcliffe wa asilimia 25 ya United hautarajiwi kupigiwa kura na bodi yao siku ya Alhamisi huku maelezo ya mwisho ya mkataba huo yakitatuliwa. (Telegraph - usajili unahitajika)

Beki wa Manchester United na Uswidi Victor Lindelof, 29, anatarajia klabu hiyo itazingatia kipengele cha kuongeza mwaka mmoja katika mkataba wake zikiwa zimesalia miezi 12 katika mkataba wake wa sasa. (90 min)

Beki wa Mashetani Wekundu na Ireland Kaskazini Jonny Evans, 35, amesema alihofia angelazimika kustaafu soka kwa sababu ya majeraha msimu uliopita kabla ya kurejea Manchester msimu wa joto. (90 min)

Aliyekuwa mkuu wa kitengo cha kuajiri wa Tottenham Paul Mitchell anapendekezwa kuwa mkurugenzi mpya wa kandanda katika klabu ya Manchester United, jambo ambalo linaweka kazi ya mkurugenzi wa sasa wa kandanda John Murtough hatarini. (The I)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
4h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
4h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
11h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
12h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
13h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
15h ago
READ MORE β†’