Robertinho anaitaka heshima kwa Al Ahly

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th October 2023


Robertinho anaitaka heshima kwa Al Ahly

Kocha wa Simba Robertinho Oliveira amesema, timu yake inakutana na mpinzani mgumu Al Ahly ukiwa ni mchezo wa mkondo wa kwanza robo fainali African Football League

Robertinho amesema wanamheshimu Al Ahly lakini kwa sasa kila mpinzani anapaswa kuiheshimu Simba pia

"Tuna timu nzuri, tunaheshimu kila mpinzani aliyepo mbele yetu, kesho ni fursa nzuri kwa wachezaji wangu kucheza mechi kubwa"

"Tunaiheshimu Al Ahly kwa sababu ina wachezaji wengi wenye uzoefu mkubwa lakini pia kila timu inapaswa kuiheshimu Simba"

"Kama nilivyosema awali Al Ahly ni timu kubwa, ina mafanikio zaidi Afrika lakini kesho tunahitaji kuonesha uwezo wetu. Kwangu mchezo wa mpira wa miguu sio kama kupigana bali ni sanaa, kesho itakuwa ni mechi nzuri," alisema Robertinho katika Mkutano na Wanahabari mapema leo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.