Mtanange wa ufunguzi African Football League kati ya Simba dhidi ya Al Ahly utapigwa saa 12 jioni katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Teknolojia ya usaidizi wa waamuzi kwa video (VAR) itatumika leo katika mchezo huo mkondo wa kwanza robo fainali
Hii ni michuano mikubwa yenye sura ya kidunia, inasimamiwa na FIFA, haishangazi kuona VAR inatumika
Maafisa waandamizi wa FIFA wakiongoza na Rais Gianni Infantino pamoja na kocha wa zamani wa Arsenal, Arsene Wenger ni miongoni mwa watu mashuhuri ambao watakuwa dimba la Mkapa leo kushuhudia ufunguzi
Patrice Motsepe ambaye ni Rais wa CAF, yeye ataongoza jopo la waandamizi kutoka CAF
Leo majira ya mchana Motsepe atazungumza na wanahabari kuweka hadharani kombe ambalo bingwa wa michuano hii atakabidhiwa
Kwa hakika hii ni siku kubwa kwa klabu ya Simba na Watanzania kwa ujumla



