Azam - Yanga - Local

Kocha Azam Fc atamba, amepata dawa ya Yanga

Joel JJ By Joel JJ
21 Oct 2023
Kocha Azam Fc atamba, amepata dawa ya Yanga

Kocha Mkuu wa Azam FC, Youssouph Dabo amewaambia wachezaji wake kuonesha thamani yao ya juu katika kila mchezo ukiwemo wa dhidi ya Young Africans utakaopigwa Jumatatu, Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es salaam

Dabo amesema anawafahamu Young Africans kwa kuwa alikutana nao kwenye mechi ya Ngao ya Jamii na kufungwa mabao 2-0 lakini anaamini hii ni mechi nyingine na amewaandaa wachezaji wake kwa namna nyingine

"Nimewaeleza wachezaji wangu tangu tumeanza msimu kwamba hatuchezi na mpinzani mmoja au wawili, tunapaswa kucheza vizuri kila wakati, kupambana na kuonesha thamani yetu kwa kushikamana na utayari kila mchezo, hilo ndio la muhimu"

"Na sasa tunakutana na Young Africans, timu ambayo tulikutana nayo Tanga (Uwanja wa Mkwakwani) katika Ngao ya Jamii, ulikuwa wakati mzuri kuwafahamu lakini huu ni mchezo mwingine na kuna utofauti tangu wakati ule na sasa hivyo tunaendelea kujiandaa tukitazamia kukua zaidi kila wakati," amesema Dabo raia wa Senegal.

Timu hizo zinakutana wakati Azam ikiwa juu kwenye nafasi ya pili kwa pointi 13 baada ya ushindi wa medhi nne na sare moja, huku Young Africans ikiwa nafasi ya tatu kwa pointi 12 ilizovuna baada ya ushindi wa mechi nne na kufungwa mchezo mmoja.

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
13h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
14h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
16h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
16h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
17h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
17h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
18h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
18h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
18h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
20h ago
READ MORE →