Simba yaiwahi Al Ahly Misri

Joel JJ By Joel JJ β€’ 22nd October 2023


Simba yaiwahi Al Ahly Misri

Msafara wa kikosi cha Simba uliwasili nchini Misri majira ya usiku wa kuamkia leo kuelekea mchezo wa mkondo wa pili robo fainali AFL dhidi ya Al Ahly

Mchezo huo utapigwa keshokutwa Jumanne nchini humo. Simba ilisafiri na msafara wa wachezaji 24 nchini Misri kuisaka nafasi ya kutinga nusu fainali dhidi ya mabingwa hao wa Afrika

Katika mchezo huo Simba itahitaji ushindi au matokeo ya sare ya kuanzia mabao 3-3 ili kutinga nusu fainali

Sare ya mabao 2-2 itapelekea mchezo huo kuamuliwa kwa changamoto ya mikwaju ya penati


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.