Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema wamejipanga kuibuka na ushindi kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa leo katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Gamondi amesema anafahamu ugumu wa mchezo huo kwani anakutana na moja ya timu bora kwa sasa Tanzania lakini lengo lake ni kuona vijana wake wanaondoka na alama zote tatu
"Tunafahamu tunakwenda kupambana na timu ngumu Azam Fc, moja ya timu bora hapa Tanzania lakini sisi tuna malengo ambayo tunahitaji kuyatimiza"
"Nafurahi tumerejea katika uwanja wa Benjamin Mkapa, ari ya kikosi iko juu, kila mmoja ana shauku kubwa ya kucheza mchezo huo," alisema
Gamondi amewataka mashabiki wa Yanga kujitokeza kwa wingi katika dimba la Benjamin Mkapa kuishangilia timu yao kwani anaamini shabiki ni mchezaji wa 12 uwanjani
Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, winga Skudu Makudubela amewataka mashabiki wa Yanga wajtokeze kwa wingi uwanjani kwani wamewaandalia burudani itakayoambatana na ushindi mnono
"Kama kocha alivyosema, tunawahitaji mashabiki waje kwa wingi kwani wao ni wachezaji wa 12. Tunafahamu mashabiki wetu wanahitaji burudani ambayo ni kushangilia magoli hivyo tunawaahidi tutawapa burudani hiyo," alisema Skudu



