Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amebainisha kuwa kikosi chake kitakuwa na mabadiliko kwenye mchezo wa mkondo wa pili robo fainali African Football League dhidi ya Al Ahly
Mchezo huo utapigwa kesho Jumanne katika uwanja wa Kimatifa wa Cairo saa 11 jioni
Akizungumza katika Mkutano na wanahabari kuelekea mchezo huo, Robertinho amesema anatambua utakuwa mchezo mgumu lakini atafanya mabadiliko muhimu katika kikosi ili kuhakikisha wanapata ushindi huko Misri
"Nafahamu ni mechi ngumu na kubwa barani Afrika, nimepanga kuingia na mpango tofauti na ilivyokuwa kwenye mchezo wa kwanza"
"Nitafanya mabadiliko ya wachezaji kwenye baadhi ya maeneo ili tuweze kucheza vizuri na kupata ushindi," alisema Robertinho
Simba inakamilisha maandalizi ya mwisho leo, mazoezi yatafanyika saa 11 jioni kwenye uwanja wa Cairo



