Robertinho kuwabadilishia mbinu Al Ahly

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd October 2023


Robertinho kuwabadilishia mbinu Al Ahly

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amebainisha kuwa kikosi chake kitakuwa na mabadiliko kwenye mchezo wa mkondo wa pili robo fainali African Football League dhidi ya Al Ahly

Mchezo huo utapigwa kesho Jumanne katika uwanja wa Kimatifa wa Cairo saa 11 jioni

Akizungumza katika Mkutano na wanahabari kuelekea mchezo huo, Robertinho amesema anatambua utakuwa mchezo mgumu lakini atafanya mabadiliko muhimu katika kikosi ili kuhakikisha wanapata ushindi huko Misri

"Nafahamu ni mechi ngumu na kubwa barani Afrika, nimepanga kuingia na mpango tofauti na ilivyokuwa kwenye mchezo wa kwanza"

"Nitafanya mabadiliko ya wachezaji kwenye baadhi ya maeneo ili tuweze kucheza vizuri na kupata ushindi," alisema Robertinho

Simba inakamilisha maandalizi ya mwisho leo, mazoezi yatafanyika saa 11 jioni kwenye uwanja wa Cairo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.