Yanga yaichapa Azam Fc 3-2

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd October 2023


Yanga yaichapa Azam Fc 3-2

Yanga imerudi kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya NBC baada ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Azam Fc katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Moja ya mechi bora kushuhudiwa kwenye ligi kuu msimu huu, mechi ikiamuliwa na mchezaji mkubwa Stephane Aziz Ki aliyefunga hat-trik

Aziz Ki alifunga bao lake la kwanza kwenye mchezo huo katika dakika ya nane baada ya kuwatoka walinzi wa Azam Fc na kuweka mpira kimiani

Azam Fc walirejea mchezoni kwenye dakika ya 18 kupitia kwa Gibril Sillah ambaye shuti lake la mguu wa kushoto lilimshinda mlinda lango wa Yanga Djigui Diarra

Hata hivyo picha za marudio zinaonyesha Sillah alipkea mpira akiwa kwenye eneo la kuotea kabla ya kupiga shuti lililojaa upande wa kushoto wa Diarra

Mpaka mapumziko timu hizo zilikuwa zimetoshana nguvu kwa sare ya bao 1-1

Yanga waliwaheshimu sana Azam Fc kwenye kipindi cha kwanza lakini vijana wa Gamondi walirejea wakiwa na moto katika kipindi cha pili

Hata hivyo ni Azam Fc waliofunga bao la pili dakika ya 63 kupitia mkwaju wa penati wa Prince Dube baada ya Sillah kuangushwa kwenye eneo la hatari na nahodha Mwamnyeto

Yanga iliongeza kasi ya mashambulizi na Aziz Ki kufunga mabao mawili ya haraka haraka kwenye dakika za 69 na 72

Alifunga bao la pili kupitia mpira wa adhabu kabla ya kuongeza la tatu baada ya pasi kutoka kwa Aucho

Ulikuwa mchezo mgumu ambao kwa hakika wachezaji wa Yanga walivuja jasho jingi kupata ushindi huo

Yanga imepanda kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 15


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.