Simba imeondoshwa kwenye michuano ya African Football League kwa kanuni ya bao la ugenini baada ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Al Ahly katika mchezo uliopigwa huko Misri leo
Moja ya mechi bora kabisa kwa kocha Robertinho Oliveira ambaye alikuja na mbinu sahihi za kuwadhibiti Al Ahly katika uwanja wao wa nyumbani
Bao la Sadio Kanoute nusura liifanye Simba irejee historia yake ya mwaka 2003 kwa kuwatoa vigogo wengine wa Misri katika mashindano
Lakini Mohammed Karhaba aliwanusuru Al Ahly na kipigo akisawazisha kwenye dakika ya 75
Mabao ya ugenini yameibeba Al Ahly kwani mchezo huo umemalizika kwa sare ya mabao 3-3 lakini Al Ahly wamefaidika kwa sababu walifunga mabao mawili kwenye mchezo wa kwanza
Lakini habari kubwa ni kile alichofanya Simba katika uwanja wa KImataifa wa Cairo. Hii inaonyesha ni kwa kiasi gani Simba iko karibu sana kufikia malengo yake ya kulitawala soka la Afrika
Al Ahly ni mabingwa wa Afrika, timu bora ya karne lakini leo walihitaji bahati na kumuomba mungu kufanikiwa kuvuka mbele ya Mnyama
Hongera kwa wachezaji na hongera kwa benchi la ufundi, huyu Robertinho imefika wakati Wanasimba wanapaswa kumuheshimu kwani ataifikisha Simba mbali sana





