Simba - Local

Al Ahly chupuchupu mbele ya Simba Misri

Joel JJ By Joel JJ
24 Oct 2023
Al Ahly chupuchupu mbele ya Simba Misri

Simba imeondoshwa kwenye michuano ya African Football League kwa kanuni ya bao la ugenini baada ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Al Ahly katika mchezo uliopigwa huko Misri leo

Moja ya mechi bora kabisa kwa kocha Robertinho Oliveira ambaye alikuja na mbinu sahihi za kuwadhibiti Al Ahly katika uwanja wao wa nyumbani

Bao la Sadio Kanoute nusura liifanye Simba irejee historia yake ya mwaka 2003 kwa kuwatoa vigogo wengine wa Misri katika mashindano

Lakini Mohammed Karhaba aliwanusuru Al Ahly na kipigo akisawazisha kwenye dakika ya 75

Mabao ya ugenini yameibeba Al Ahly kwani mchezo huo umemalizika kwa sare ya mabao 3-3 lakini Al Ahly wamefaidika kwa sababu walifunga mabao mawili kwenye mchezo wa kwanza

Lakini habari kubwa ni kile alichofanya Simba katika uwanja wa KImataifa wa Cairo. Hii inaonyesha ni kwa kiasi gani Simba iko karibu sana kufikia malengo yake ya kulitawala soka la Afrika

Al Ahly ni mabingwa wa Afrika, timu bora ya karne lakini leo walihitaji bahati na kumuomba mungu kufanikiwa kuvuka mbele ya Mnyama

Hongera kwa wachezaji na hongera kwa benchi la ufundi, huyu Robertinho imefika wakati Wanasimba wanapaswa kumuheshimu kwani ataifikisha Simba mbali sana

More Stories

Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
52m ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
55m ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
1h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
1h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
1h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
3h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
13h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
13h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
14h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
17h ago
READ MORE →