Wagosi wa Kaya Coastal Union wamezinduka katika uwanja wa nyumbani, Mkwakwani wakiibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mashujaa Fc katika mchezo wa ligi kuu ya NBC
Mabao ya Bakari Selemani na Lucas Kikoti (p) yaliihakikishia Coastal Union ushindi wao wa kwanza msimu huu
Coastal Union wangeweza kuibuka na ushindi mnono zaidi wakipoteza nafasi nyingine kupitia mkwaju wa penati
Huo ulikuwa ushindi wa kwanza kwa Coastal Union msimu huu pia wakifunga kwenye uwanja wa nyumbani kwa mara ya kwanza msimu huu
Mashujaa Fc iliyoanza vyema msimu, leo imepoteza mchezo wa pili mfululizo
Aidha JKT Tanzania nayo ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Tabora United katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex mapema
Bao pekee la JKT Tanzania lilifungwa na Maka Edward kwenye dakika ya 17



