Simba yaendeleza ubabe Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th October 2023


Simba yaendeleza ubabe Ligi Kuu

Mnyama Simba Sc ameunguruma uwanja wa Benjamin Mkapa akiendeleza rekodi ya ushindi kwa asilimia 100 msimu huu baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ihefu

Dhamira ya Simba kuusaka ubingwa imeendelea kudhihiri kwa wababe hao wa soka ukanda wa Afrika Mashariki kuendelea kushusha vipigo kwa kila anayekuja mbele

Haukuwa mchezo mwepesi kwa vijana wa Robertinho lakini suala la alama tatu ndio matokeo waliyohitaji na walifanikiwa kuyapata

Jean Baleke aliitanguliza Simba kwa kufunga bao la kwanza dakika ya 13 akitumia makosa ya safu ya ulinzi ya Ihefu Fc

Walima mpunga hao kutoka Mbarali wakarejea mchezo kwa kusawazisha bao kupitia kwa Ismail Juma kabla ya Moses Phiri hajaihakikishia Simba alama tatu muhimu ambazo zimewafanya wafikishe alama 18 sawa na Yanga lakini Simba ikiwa na mechi moja ya kiporo

Phiri ameendelea kuonyesha thamani yake licha ya kutopata muda mrefu wa kucheza. Phiri amefikisha mabao matatu msimu huu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.