Tangu msimu uliopita, klabu ya Azam Fc iliweka utaratibu wa mashabiki kuingia bure kushuhudia mechi za timu hiyo zinazopigwa uwanja wa Azam Complex
Shabiki alitakiwa kuvaa jezi yoyote ya Azam na kuruhusiwa kuingia Azam Complex kushuhudia mechi ya matajiri hao kutoka Chamazi
Hata hivyo utaratibu huo haukuwepo kwenye mchezo uliopita wa ligi kuu dhidi ya Namungo Fc, mashabiki walitakiwa kulipa viingilio
Mashabiki wachache wakaingia kushuhudia mchezo huo ambao Azam Fc walikubali kipigo cha mabao 3-1 nyumbani
Afisa Habari wa Azam Fc Hasheem Ibwe amethibitisha kuwa kuanza sasa mashabiki watatakiwa kulipa viingilio kama ilivyokuwa zamani
Pamoja na kuwa hakutaka kuweka wazi kwa nini wamebadili utaratibu, imeelezwa kuwa moja ya sababu ni zomea zomea wanayokutana nayo Azam Fc kutoka kwa mashabiki
Idadi kubwa ya mashabiki ambao wamekuwa wakiingia bure sio wa Azam Fc, mara nyingi hushangilia timu pinzani badala ya Azam



