Simba yatangaza viingilio Kariakoo Derby

Joel JJ By Joel JJ β€’ 30th October 2023


Simba yatangaza viingilio Kariakoo Derby

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally ametangaza viingilio vya mchezo wa ligi kuu ya NBC kati ya Simba dhidi ya Yanga ambao utapigwa Jumapili, Novemba 05 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo, Ahmed alisema Simba inahitaji ushindi katika mchezo huo, mashabiki wamekuwa silaha muhimu kwa Simba, Jumapili wanahitajika kwa wingi wao

"Ni mechi ambayo Wanasimba inabidi tujitoe muhanga ili kupata ushindi. Kila Mwanasimba ajue ana jukumu la kusaidia timu yake. Tukishinda siku hiyo shughuli itakuwa imeisha, itabaki shughuli ya kukamilisha ratiba ya msimu"

"Raha ya msiba waliaji wawe wengi, tunawaomba mashabiki wao waje uwanjani na wakae hadi mwishoni sio tukishawafunga wawahi kuondoka, wasubiri hadi mchezo uishe"

"Viingilio Mzunguko - Tsh. 5,000, Machungwa - Tsh. 10,000, VIP C - Tsh. 20,000, VIP B - Tsh. 30,000, VIP A - Tsh. 40,000 na Platinum - Tsh. 150,000," alisema Ahmed

Adha Ahmed amebainisha kuwa kikosi cha Simba kinatarajiwa kuingia kambini kesho Jumanne kwa ajili ya maandalizi ya mchezo huo

"Kikosi kitaingia kambini kesho Jumanne, kwa kawaida mechi za ndani huwa tunaingia siku tatu kabla ya mchezo lakini hii tunawahi. Tumeutolea macho mchezo huu kuhakikisha tunapata ushindi."

"Kocha wao ameshakuja kwenye mechi tatu hadi sasa na leo tunatangaza kumkaribisha kwenye mazoezi yetu yatakayofanyika Mo Simba Arena. Tunamualika rasmi aje siku yoyote anayotaka."

"Sisi hatuna jambo dogo hivyo tutafanya hamasa, ni mchezo wetu, tutautangaza tutakavyo tunajua watu watakuja lakini lazima tuichangamshe. Tutakuwa na wiki ya mchakamchaka wa kuaga kwao aage atarudi Jumatatu ya Novemba 6, 2023," alitamba Ahmed


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.