Real Madrid wako tayari kujadiliana na Chelsea kuhusu mkataba wa kudumu wa Kepa Arrizabalaga, lakini hawatalipa zaidi ya euro milioni 17.5 kwa kipa huyo Mhispania mwenye umri wa miaka 29 ambaye aliigharimu The Blues takriban euro milioni 71.6 miaka mitano iliyopita. (Sun)
Juventus huenda ikatumia mshahara uliookolewa kwa kiungo wa Ufaransa Paul Pogba, 30, kumpata kiungo wa Arsenal Thomas Partey, 30, katika mkataba wa mkopo mwezi Januari. Pogba anakabiliwa na adhabu ya kufungiwa kwa muda mrefu kutojihusisha na soka ambayo itasababisha kupunguzwa kwa mshahara kutoka kwa Juve. (Mirror)
Mkufunzi wa Arsenal Mikel Arteta ameripotiwa kuwaongeza viungo Martin Zubimendi, 24, wa Real Sociedad na Uhispania na Aurelien Tchouameni, 23, wa Real Madrid na Ufaransa kwenye orodha ya walengwa wa kuhama. (Calciomercato - kwa Kihispania)
Chelsea wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Ujerumani Florian Wirtz kutoka Bayer Leverkusen huku Manchester City pia wakimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20. (Express)
Chelsea ilituma maskauti kumtazama mlinda mlango wa Georgia na Valencia Giorgi Mamadashvili, 23, kwenye mechi ya timu hiyo ya Uhispania ugenini Granada Jumapili. (90 min)
Kocha wa The Blues Mauricio Pochettino pia anavutiwa na kipa wa Athletic Bilbao na Uhispania Unai Simon, 26. (Fichajes - kwa Kihispania)
Napoli wako tayari kufanya mazungumzo ya mkataba mpya na mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen huku Liverpool wakihusishwa na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (Fichajes - kwa Kihispania)
Beki wa Chelsea na England Trevor Chalobah, 24, amevutiwa na Borussia Dortmund. (Sun)
Mshambuliaji wa kimataifa wa Uingereza Divin Mubama, 19, amekataa kuongezewa mkataba katika klabu ya West Ham ikiwa imesalia mwaka mmoja katika mkataba wake wa sasa. (the athletic- Usajili unahitajika)
BBC



