Al Hilal kutumia uwanja wa Benjamin Mkapa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 31st October 2023


Al Hilal kutumia uwanja wa Benjamin Mkapa

Klabu ya Al Hilal ya Sudan imetangaza rasmi kutumia Uwanja wa Mkapa uliopo Dar es Salaam, Tanzania katika mechi za hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika

Al Hilal ipo kundi moja na timu za ES Tunis, Etoile Sportive du Sahel za Tunisia na Atletico Petroleos ya Angola

Kupitia akaunti yao rasmi ya Instagram wameishukuru TFF kwa kuwakubalia ombi lao la kutumia uwanja huo wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 60,000

Al Hilal iliweka kambi nchini Morocco ikikimbia vita vinavyoendelea huko Sudan

Al Hilal imeungana na klabu za Simba na Yanga ambazo pia zinatumia uwanja wa Benjamin Mkapa katika mechi zao za ligi ya mabingwa hatua ya makundi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.