Mazungumzo kati ya Manchester United na beki wao Aaron Wan-Bissaka kuhusu mkataba mpya yanaonekana kukwama. United sasa wanafikiria kutumia kifungu cha nyongeza ya miezi 12 katika mkataba wa sasa wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Daily Mail)
Manchester United wanapania kumnunua mlinzi wa Chelsea Trevoh Chalobah, huku Muingereza huyo mwenye umri wa miaka 24 akiambiwa kuwa hayumo katika mipango ya Mauricio Pochettino. (Teamtalk)
Brentford wako tayari kumuuza Ivan Toney, 27, mwezi Januari na wameweka bei ya pauni milioni 80 kwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uingereza. (Evening Standard)
Liverpool wanamnyatia mlinzi wa Ajax Devyne Rensch, 20, lakini wanaweza kukabiliwa na ushindani kutoka kwa Arsenal kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi. (Football Insider)
Newcastle United wameanza mazungumzo na Santos kuhusu usajili wa mshambuliaji wa Brazil Marcos Leonardo, 20, ambaye anakadiriwa kuwa £25m, mwezi Januari. (UOL - kwa Kireno)
Wolves, West Ham na Leeds wanashindania winga wa Fluminense wa Colombia Jhon Arias mwenye umri wa miaka 26. (Teamtalk)
Manchester United ilituma maskauti kumtazama mlinda mlango wa Ureno Diogo Costa, 24, akiichezea Porto dhidi ya Vizela siku ya Jumapili. (A Bola - kwa Kireno)
Arsenal, Chelsea na Real Madrid wanawania kumsajili winga wa Ireland Naj Razi mwenye umri wa miaka 17 kutoka Shamrock Rovers. (Sun)
Winga wa Brazil Rodrygo, 22, anatazamiwa kusaini mkataba mpya na Real Madrid hadi 2028, licha ya akiwa kuhusishwa na Liverpool na Paris St-Germain hivi majuzi. (Fabrizio Romano)
Mshambulizi wa Barcelona wa Uhispania Ansu Fati, 21, ambaye yuko Brighton kwa mkopo, anavutia vilabu vya Saudi Arabia. (Estadio Deportivo - kwa Kihispania)
Everton wako tayari kuchuana na Roma na Lazio kwa ajili ya kuinasa saini ya winga wa Italia Wilfried Gnonto, 19, ambaye alijaribu kulazimisha kuondoka Leeds msimu wa joto. (Teamtalk)
Mshambuliaji wa Argentina Lautaro Martinez, 26, anasema anaridhika kuwa katika klabu ya Inter Milan ya Italia, licha ya kuhusishwa na Real Madrid ya Uhispania. (Sky Sports)
BBC



