Simba - Local

SBL kuidhamini Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 Nov 2023
SBL kuidhamini Simba

Kampuni ya Serengeti Breweries Limited (SBL) kupitia Pilsner Lager, imesaini mkataba wa miaka mitatu kuidhamini klabu ya Simba

Mkataba huo wenyewe thamani ya Tsh Bilioni 1.5, ulisainiwa katika hafla iliyofanyika mapema leo

Mtendaji Mkuu wa Simba Imani Kajula amesema udhamini huo umekuja wakati muafaka na utasaidia katika gharama za uendeshaji wa klabu

"Ni ubia wa nguvu kabisa, ubia wa Simba wawili. Hii ni package ambayo imekuja wakati mwafaka. Serengeti ni mbia mkubwa sana wa mpira wa Tanzania, huu ni mwendelezo wa kusaidia mpira"

"Udhamini huu utasaidia uendeshaji wa klabu, gharama za uendeshaji wa vilabu huwa ni kubwa. Upatikanaji wa fedha ni muhimu sana. Tunawashukuru kukubali kuungana nasi kama wadhamini wa Simba," alisema Kajula

Nae Meneja wa Masoko wa SBL, Anitha Rwehumbiza amesema ushirikiano huo utaifanya Serengeti ishiriki matukio mbalimbali ya Simba kuanzia mchezo wa dabi dhidi ya Yanga siku ya Jumapili na mechi nyingine zitakazopigwa Dar es salaam na nje ya Dar es salaam

"Tulikuwa na lengo la kupata mshirika ambaye ana mashabiki wengi, na tulikuwa na furaha tulipopata taarifa kwamba Simba ipo tayari"

"Ukiacha kwamba Simba na Pilsner zinaendana kwa rangi na Simba pia Nguvu Moja ya Simba ni ya kuunganisha Watanzania wote na kinywaji chao cha Pilsner Lager."

"Tutaanza kushiriki matukio ya Simba kwa kuanzia na derby na hata michezo za nje ya Dar. Kwetu ilikuwa na ndoto lakini tunafurahi tumekuja kwa muda sahihi. Tutatumia watu wa vyombo vya habari na tutakuwepo uwanjani kuitangaza Pilsner Lager na Simba," alisema

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
31m ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
10h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
10h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
11h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
18h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
19h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
20h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
20h ago
READ MORE β†’