Mchezo wa fainali ya michuano ya African Football League, utazikutanisha Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini dhidi ya Wydad Athletic ya Morocco
Fainali hiyo itakuwa kumbukumbu ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa msimu uliopita Wydad wakitinga fainali kwa faida ya mabao ya ugenini baada ya sare ya mabao 2-2 dhidi ya Sundowns katika mchezo uliopigwa Afrika Kusini. Mchezo wa kwanza uliopigwa Morocco ulimalizika kwa sare ya bao 1-1
Mchezo wa kwanza wa fainali utapigwa Novemba 05 huko Morocco na mechi ya marudiano kupigwa Novemba 11 nchini Afrika Kusini
Wydad walitinga fainali ya michuano hiyo kwa ushindi wa mikwaju ya penati 5-4 dhidi ya Esperance baada ya kuchapwa bao 1-0 na Esperance katika mchezo wa nusu fainali mkondo wa pili. Wydad walishinda bao 1-0 kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza
Mamelodi wao waliwatupa nje Al Ahly baada ya kuwalazimisha suluhu ya bila kufungana huko Misri, Mamelodi wakishinda bao 1-0 kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza
Al Ahly waliponea chupuchupu mbele ya Simba ya Tanzania katika robo fainali wakitinga nusu fainali kwa faida ya mabao ya ugenini baada ya sare ya mabao 3-3 katika mechi zote mbili za robo fainali




